Mhe. Mchengerwa- Tanzania na Real Madrid wajadili ushirikiano katika michezo.

 



Na John Mapepele

Waziri wa Utamaduni, Sanaa na Michezo, Mhe. Mohamed Mchengerwa amefanya majadiliano ya awali na uongozi wa juu wa Klabu ya Real Madrid ya Hispania kuhusu kufanya ushirikiano katika kukuza vipaji vya Soka baina ya Klabu hiyo na  Tanzania.

Mazungumzo hayo  yamefanyika leo Oktoba 10, 2022 kwa njia ya mtandao ambapo wamejadili  kufanya uwekezaji mkubwa kwenye kuibua vipaji vya wachezaji wachanga na kuwakuza kuanzia kwenye akademi za michezo.

Mhe. Mchengerwa amesema Klabu hiyo imekubali  kushirikiana na  Tanzania  kuendeleza vipaji vya vijana ili kuwapata wachezaji bora wa kimataifa  kwa manufaa ya pande zote mbili. 

Mbali na kufanya uwekezaji mkubwa katika kuibua vipaji, pia imejadiliwa kushirikiana katika  kutumia michezo kutangaza utalii  wa Tanzania kwa kutumia mitandao mbalimbali ya Klabu hiyo kongwe duniani.

Mhe. Mchengerwa amesema Tanzania ina fursa  kubwa  ya kutumia michezo kuitangaza nchi kimataifa na kuinua uchumi wake

Comments

Popular posts from this blog

ZANZIBAR YANG’ARA MBIO FUPI KWENYE TAMASHA LA MICHEZO YA WANAWAKE LA TANZANITE

Mhe. Mchengerwa- Serikali kuwashirikisha wadau kwenye mnyororo wa thamani wa utalii