Hafla ya kuiaga Serengeti Girls, Mhe. Mchengerwa atoa maagizo mazito kwa Mkurugenzi mpya wa Michezo

 

Na John Mapepele

Waziri wa Utamaduni, Sanaa na Michezo, Mhe.  Mohamed Mchengerwa leo Septemba 21, 2022 amewaongoza watanzania kuiaga timu ya Serengeti Girls  kwenda Kombe la Dunia huku akitoa maelekezo mahususi kwa Kaimu Mkurugenzi mpya wa Michezo kuhusu kuendeleza sekta hiyo.

Katika hafla ya kuiaga timu hiyo iliyofanyika jijini Dar es Salaam, Mhe. Mchengerwa amekabidhi BIMA na  vifaa mbalimbali  vya michezo ambapo pia Katibu Mkuu wa Wizara hiyo Dkt. Hassan Abbasi  na wadau mbalimbali wa michezo walishiriki.

Mhe. Mchengerwa  amemtaka Kaimu Mkurugenzi mpya, Ally  Mayay kuleta maboresho kusudiwa kwenye Sekta ya Michezo na endapo hataweza ataondolewa.

Mbali na hayo,  Mhe. Mchengerwa amempa  maelekezo  mahususi ambayo ametaka yafanyiwe kazi mara moja.

Maelekezo hayo ni pamoja na kuweka mfumo wa Kutafuta vipaji vya wachezaji Kwa kushirikiana na Baraza la Michezo la Taifa ( BMT) na  Shirikisho la Soka nchini (TFF) pia kuandaa  mifumo ya kuwasajili wanamichezo kuanzia ngazi za Umitashumta na Umiseta na kuendelea  kuwalea.

Ashirikiane na Wizara wadau  wa michezo, kama TAMISEMI, Elimu  ili kuja na mpango  wa kuifanya michezo kuwa sehemu ya masomo ya nayofundishwa mashuleni.

Maelekezo mengine nikuboresha miundombinu ya michezo ikiwa ni pamoja na kukarabati viwanja vitano vya Soka ambavyo Serikali inakusudia kufanya ukarabati  ili Tanzania iweze kufuzu  kuratibu mashindano ya AFCON mwaka 2027.


Amesema dhamira ya Serikali na ndoto za Mhe. Rais Samia Suluhu Hassan ni kuona kuwa Tanzania inaratibu mashindano hayo na hatimaye kombe la dunia.

Pia amemtaka aandae mara moja  kanzidata ya walimu na wakufunzi wa michezo

Aidha, amemtaka kushirikisha  wadau hususan  balozi ambazo zipo tayari na mipango kazi ya kusaidia kujenga miundombinu ya michezo nchini.

Kwa upande wake, Ally Mayay amemshukuru Mhe. Waziri Mchengerwa kwa kumteua na kuahidi kufanyia kazi maelekezo yote yaliyotolewa.


Comments

Popular posts from this blog

ZANZIBAR YANG’ARA MBIO FUPI KWENYE TAMASHA LA MICHEZO YA WANAWAKE LA TANZANITE

Mhe. Mchengerwa- Serikali kuwashirikisha wadau kwenye mnyororo wa thamani wa utalii