Waziri Mchengerwa aelekeza vilabu vyote kumiliki viwanja vyake vyenyewe, Yanga na Simba vyaahidi kutekeleza agizo hilo ndani ya miezi sita.

 

Na John Mapepele

Waziri wa Utamaduni, Sanaa na Michezo, Mhe. Mohamed Mchengerwa leo Agosti 17, 2022 ameelekeza vilabu vyote kumiliki viwanja vyake vyenyewe ambapo timu ya  Yanga na Simba zimeahidi kutekeleza agizo hilo ndani ya miezi sita. 

Mhe. Mchengerwa ameyasema hayo  alipokutana na  watendaji wakuu wa vilabu vinavyoshiriki ligi kuu  jijini Dar es Salaam na  kujadili  namna bora ya kuendesha ligi   kwa ubunifu na ushindani wa hali ya juu ili kuifanya ligi iwe na mvuto.

Mhe. Mchengerwa amesema mpango wa vilabu kumiliki  viwanja vyao  ni takwa la kisheri kulingana na Sera ya Michezo nchini.

Aidha, Mhe. Mchengerwa amefafanua kuwa  pamoja na mambo mengine kikao hicho kimejadili masuala ya kuzingatia  weledi, nidhamu na maadili.


Amesema kwa sasa Serikali haiwezi kukubaliana na vitendo vyovyote vya rushwa na upendeleo katika michezo kwa kuwa vinasaidia kuua na kudidimiza michezo.

Amesema dhamira ya Serikali  kwa sasa ni kuendesha michezo kisasa ili kuleta maboresho makubwa yatakayosaidia kuifikisha Tanzania kwenye ramani ya kimataifa.

Viongozi hao  wamemshukuru Waziri Mchengerwa kwa kuja na mpango  huo wa kuwashirikisha  viongozi ili waweze kujadili changamoto zao na Serikali na kupata ufumbuzi wa pamoja na wa kudumu.




Comments

Popular posts from this blog

ZANZIBAR YANG’ARA MBIO FUPI KWENYE TAMASHA LA MICHEZO YA WANAWAKE LA TANZANITE

Mhe. Mchengerwa- Serikali kuwashirikisha wadau kwenye mnyororo wa thamani wa utalii