Popular posts from this blog
ZANZIBAR YANG’ARA MBIO FUPI KWENYE TAMASHA LA MICHEZO YA WANAWAKE LA TANZANITE
Na John Mapepele, Dsm Zanzibar imeibuka mbabe katika mashindano ya mbio fupi uwanja wa Benjamini Mkapa kwenye maadhimisho yanayoendelea ya Tamasha la Michezo ya Wanawake la Tanzanite leo Septemba 17, 2021ikiwa ni siku ya pili kabla ya kuzinduliwa rasmi kesho na Mhe. Rais Samia Suluhu Hassan Kwa mujibu wa Mkurugenzi wa uratibu wa mbio hizo, Robert Kalyahe amesema Zanzibar imeweza kuwa bingwa kwa mbio za mita mia moja katika nafasi zote tatu ambapo amesema mshindi wa kwanza kwenye mbio hizo ni Hynes Jolini aliyetumia sekunde 11:62 akifuatiwa na Winfrida Makenji aliyetumia sekunde 11:74 na nafasi ya tatu imekwenda kwa Kazija Hassan aliyetumia sekunde12:45. Pia Kalyahe amesema katika mbio za mita mia mbili nafasi zote tatu zimenyakuliwa na washindi kutoka Zanzibar ambapo amesema Emma Hossea amenyakua nafasi ya kwanza kwa kutumia sekunde 24:82 na nafasi ya pili imechukuliwa na Nasra Abdallah aliyetumia sekunde 25:55 wakati nafasi ya tatu imekwenda kwa Neema Ally a...
Mhe. Mchengerwa- Serikali kuwashirikisha wadau kwenye mnyororo wa thamani wa utalii
Na John Mapepele Waziri wa Maliasili na Utalii, Mhe. Mohamed Mchengerwa amesema Serikali imedhamiria kufanya kazi kwa pamoja na wadau mbalimbali wa utalii nchini kwa ajili ya kuimarisha mahusiano ya serikali na wadau (Public Private Partnership) ili kufikia kwa haraka lengo la kuwapata watalii milioni tano hatimaye kuchangia kwenye uchumi wa nchi. Akizungumza kwenye Tamasha la Kwanza la Biashara la Wadau wa Utalii leo, Februari 23, 2023 lililopewa jina la “The Z sumit” ambapo Rais wa Zanzibar, Mhe. Hussein Mwinyi amekuwa Mgeni Rasmi, Mhe. Mchengerwa amesisitiza kuwa dhamira ya serikali kwa sasa ni kuwashirikisha wadau wote kwenye mnyororo wa thamani wa utalii ili kutoa huduma ya kiwango cha kimataifa kitakachowavutia watalii kuja kujionea vivutio mbalimbali vya utalii hapa nchini. Aidha, amemhakikishia Mhe. Rais Mwinyi kufanya kazi kwa karibu na Waziri anayesimamia sekta ya Utalii kwa upande wa Zanzibar katik...
Comments
Post a Comment