Posts

Showing posts from April, 2021

KAMATI YA MAKATIBU WAKUU YAANDAA MKAKATI KABAMBE WA KUBORESHA MICHEZO MASHULENI

Image
  Kamati ya Makatibu Wakuu wa Wizara zenye dhamana yaElimu,Michezo na TAMISEMI  wakiwa kwenye kikao  kazi leo Aprili 27,2021 Jijini Dodoma kujadili utekelezaji wa maelekezo ya Mawaziri wenye dhamana hizo hizo kwa lengo la   kuandaa Mkakati wa Utekelezaji wa masuala mbalimbali ya uimarishaji wa somo la Elimu kwa Michezo na Michezo katika shule za Msingi na Sekondari hapa nchini chini ya uenyekiti wa Prof.Riziki Shemdoe ambaye ni Katibu Mkuu wa Wizara ya  TAMISEMI. Dkt. Hasssan Abbasi, Katibu Mkuu wa Wizara ya Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo (kushoto) na Naibu Katibu Mkuu TAMISEMI anayeshughulikia eneo la Elimu ndugu  Gerard Mweli (kulia) wakihudhuria kikao cha Kamati ya Makatibu Wakuu wa Wizara zenye dhamana ya Elimu, Michezo na TAMISEMI  wamefanya kikao kazi leoAprili 27,2021Jijini Dodoma kujadili utekelezaji wa maelekezo ya Mawaziri wenye dhamana hizo hizo kwa lengo la   kuandaa Mkakati wa Utekelezaji wa mas...

SERIKALI YAANZISHA KITUO CHA KIMATAIFA CHA KUENDELEZA VIPAJI VYA MICHEZO.

Image
    Mkurugenzi wa Idara ya Maendeleo ya Michezo nchini, Yusuph Singo Omari (kushoto), akiwa naa liyewahi kuwa Mkurugenzi wa Ufundi wa TFF na Kocha wa Timu ya Taifa Stars, Ami Ninje (katikati) na Mwenyekiti wa Bodi ya Ushauri wa Chuo cha Maendeleo ya Michezo Malya Dkt. Richard Masika wakikagua eneo la chuo kwa ajili ya mradi wa upanuzi wa chuo hicho ili kujenga Kituo cha kuendeleza vipaji vya michezo. Timu ya wataalam mbalimbali wa michezo na ardhi ikipitia ramani ya maeneo ya ujenzi wa madarasa na hosteli. Timu ya wataalam ikiangalia eneo la ujenzi wa madarasa wa Kituo cha kuendeleza vipaji vya Michezo   Na John Mapepele, Dodoma   Serikali inatekeleza mradi wa  kupanua eneo la  Chuo cha  Maendeleo ya Michezo Malya ikiwa ni  mkakati  maalum wa kuanzisha Kituo cha Kuendeleza Vipaji vya Michezo  ili kuibua na kuendeleza vipaji vya wanamichezo hapa nchini.   Mkurugenzi wa Idara ya Maendeleo ya Michezo nchin...

WAITARA ATAKA MASLAHI BORA KWA WATUMISHI

Image
  Naibu Waziri wa Ujenzi na Uchukuzi, Mwita Waitara, akisisitiza jambo kwa wajumbe wa Baraza la Wafanyakazi la Sekta ya Uchukuzi (hawapo pichani), alipofunga baraza hilo lililokaa kwa siku mbili kujadili mpango wa bajeti ya sekta hiyo kwa mwaka wa fedha 2021/2022, jijini Dodoma. Wajumbe wa Baraza la Wafanyakazi la Sekta ya Uchukuzi, wakiimba wimbo wa mshikamano kabla ya Naibu Waziri wa Ujenzi na Uchukuzi, Mwita Waitara (hayupo pichani) kufunga baraza hilo lililokutana kwa siku mbili mjini Dodoma. Naibu Waziri wa Ujenzi na Uchukuzi, Mwita Waitara (katikati waliokaa), akiwa katika picha ya pamoja na wajumbe wa Baraza la Wafanyakazi la Sekta ya Uchukuzi mara ya kufunga baraza hilo lililofanyika jijini Dodoma. PICHA NA WUU ************************** Naibu Waziri wa Ujenzi na Uchukuzi, Mwita Waitara, amewataka watendaji wa Sekta ya Uchukuzi na Taasisi zake kuhakikisha wanajali watumishi kwa kusimamia kanuni, taratibu na sheria ili kupata matokeo chanya katika utendaji. Akizungumza mara ...

WAZIRI JAFO KUKUTANA NA WAWEKEZAJI NCHINI KUSIKILIZA KERO ZAO KUHUSIANA NA UCHELEWAJI WA VIBALI VYA TATHMINI YA ATHARI KWA MAZINGIRA(EIA)

Image
  *************************** Waziri wa Nchi Ofisi ya Makamu wa Rais Muungano na Mazingira, Mhe. Selemani Jafo, amesema kuwa anataka kukutana na wawekezaji wote Nchini siku ya Jumamosi 17/4/2021, ili kusikiliza changamoto mbalimbali zinazowakabili wawekezaji hao wakati wa kufanya Tathmini ya Athari kwa Mazingira (EIA), mkutano huo utafanyika Millenium Tower Jijini Dar es Salaam. Ameyasema hayo alipofanya ziara katika Ofisi za Baraza la Taifa la Hifadhi na Usimamizi wa Mazingira (NEMC), Makao Makuu Mikocheni Jijini Dar es Salaam baada ya uteuzi, akiwa ameambatana na Naibu Waziri wake Mhe. Hamad Chande, amesema kuwa kuna malalamiko mengi ameyapata baada ya kuteuliwa juu ya NEMC hasa kwenye mchakato wa utoaji wa Cheti cha tathmini ya Mazingira “Nimeitisha mkutano huu kutokana na malalamiko ya wawekezaji wengi kulalamikia NEMC ndio chanzo cha ucheleweshwaji wa vibali, hivyo kupelekea wawekezaji kushindwa kufanya uwekezaji katika Taifa letu. Hili suala linaathari yake kama mwekezaji ana...

MAWAZIRI WATEKELEZA AGIZO LA RAIS SAMIA SULUHU KIKAMILIFU

Image
  Naibu Waziri wa Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo Pauline Gekul (kushoto) akizungumza leo katika kikao cha Mawaziri wa Wizara ya Mawasiliano na Teknolojia ya Habari pamoja na Wizara hiyo cha kujadili hoja zinazohusu utekelezaji wa majukumu ya Sekta hizo ya kisera, kisheria na kikanuni kwenye masuala ya mawasiliano nchini kilichofanyika jijini Dodoma, anayefuata ni Waziri wake Innocent Bashungwa akifuatiwa na Waziri waMawasiliano na Teknolojia ya Habari Dkt. Faustine Ndugulile na kuliani Naibu wake Mhandisi Kundo Mathew. Kikao hicho kimefanyika kufuatia maelekezo yaliyotolewa hivi karibuni na Mheshimiwa  SamiaSuluhu Hassan, Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania  yakutaka kufanyika marekebisho ya Sheria na Kanuni zinazosimamia Vyombovya Habari  hapa nchini hususan Televishen Mtandao (Online TV)   Wajumbe wa kikao cha Mawaziri wa Wizara ya Mawasiliano na Teknolojia ya Habari pamoja naWizara ya Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo wakimsikiliza Katibu...

MHE GEKUL AOMBA USHIRIKIANO BAINA YA VIONGOZI WAKUU WA WIZARA,WATENDAJI NA WATUMISHI

Image
  Waziri wa Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo Mhe.Innocent Bashungwa (katikati mwenye tai nyekundu) akiwa  na Katibu Mkuu wa Wizara hiyo, Dkt Hassan Abbasi (mwenye tai ya bluu) wakimkaribisha Naibu Waziri, Mhe. Pauline Gekul alipowasili rasmi kwenye Ofisi yake mpya iliyopo eneo la Mji wa Serikali –Mtumba jijini Dodoma leo, baada ya kuapishwa na Mhe.Rais Samia Suluhu Hassan Aprili 01,2021 Ikulu ya Chamwino  kushika wadhifa huo. Naibu Waziri wa Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo Pauline Gekul akipokea maua kutoka  kwa wafanyakazi wa Wizara hiyo  kama ishara ya kumkaribisha rasmi kwenye Ofisi yake mpya iliyopo  eneo la Mji wa Serikali –Mtumba jijini Dodoma leo, baada ya kuapishwa  na Mhe.Rais Samia Suluhu Hassan Aprili 01,2021 Ikulu ya Chamwino  kushika wadhifa huo a.      Naibu Waziri wa Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo Pauline Gekul akisaini kitabu  cha wageni  mara baada ya kuingia kwenye Ofisi yake mpya iliyopo...